Saturday, November 6, 2010

Kikwete Aapishwa Kuwa Rais 2010 - 2015

HAYA. Mambo yanaelekea yamekwisha, leo JK ameapishwa baada ya kuchaguliwa na 27% ya watanzania waliojiandikisha kupiga kura, na 61% ya wale waliojitokeza kupiga kura!

Hapo hakuna cha kujivunia, ila kushukuru Mungu tu kuwa labda wale ambao hawakujitokeza wangepigia upinzani!

Nawapa pole wanafunzi wote wa vyuo, kwani hawakuweza kupiga kura baada ya serikali kuamua vyuo visifunguliwa hadi uchaguzi uishe ilhali wanafunzi wengi walijiandikisha wakati wakiwa chuoni. Nina hakika wengi walikuwa wanataka mabadiliko.

Ndio mwanzo huu, tunasubiri sasa mambo ya kukata rufaa na muda wa kuanza serikali mpya, tukiwa na matumaini kutakuwa na mabadiliko makubwa kiutendaji, na baadhi ya watu kupoteza ubunge wao kupitia mahakama.

Picha kutoka michuzi

3 comments:

EDNA said...

Tusubiri hiyo serikali yake mpya kama itakuwa na mabadiliko au ndiyo yatakuwa yaleyale.

emu-three said...

Kama alivyonena Edna, cha kusubiri ni hiyo nguvu kazi ya utendaji wa ahadi zilizosikika kwenye kampeni!

Upepo Mwanana said...

Hope haitakuwa ya kulindana nk. Maana dalili za moto ni Moshi, nahisi tumeanza kuona moshi mahali fulani. Ngoja tusubiri