Monday, March 28, 2011

Have a Blessed Week!

For those who never had a glimpse of enjoyable weekend..
I just say ...... "After long and tiring weekend, may Almight God bless you for the whole of this week"
For those who are Christian believers.... I wish you the best and great humiliations ... during the lent period.

Have my blessings too!
Hata kikombe cha babu kinaaminika kuponya :-)

Thursday, March 24, 2011

Kuwa Mwangalifu Katika Ujana wako

Fiona Walker bado anajutia picha hii aliyopigwa mwaka 1976 akiwa bado ni kijana wakati huo akiwa na miaka 18 tu.  
Alikubali kupiga picha hiyo kumfurahisha mpenzi wake wa kiume ambaye alikuwa na tamaa ya kuwa mpiga picha maarufu.
Ilibidi aazime nguo na reki ya mchezo wa tenisi ili aonekane kama kweli alikuwa mchezaji mahili.     
    
Rafiki yake wa kiume aliweza kupata pauni kama laki mbili na nusu kwa kuruhusu kuuzwa kwa picha hiyo ambayo ilitolewa nakala kama milioni 2 baada ya kuonekana ilikuwa maarufu sana.  
  
Sasa hivi Fiona akiiona picha hii, anajuta na kusema kama angejua, katu asingekubali kupiga picha hiyo.  
  
Soma habari hii hapa

Monday, March 21, 2011

Tanzania: Chama Tawala ni kipi?

Naomba kusaidiwa kwenye utata huu.
Nifahamuvyo mimi, ni kuwa chama tawala ni kile kinachoshikilia dola, kwa maana ya kwamba ndicho kinachotoa kiongozi mkuu mwenye mamlaka ya serikali. Kwa maana nyingine ndio kiongozi wa kiserikali wa nchi hiyo. Ambaye anafanya kazi kwa mujibu wa sheria na katiba.
Hata kwenye nchi zinazo ongozwa kifalme (na kimalkia pia).
Vyama vya upinzani vina wajibu mmoja mkuu, nao ni kukisoa chama tawala pale kinapo endesha mambo ndivyo sivyo....

Kwa Tanzania mimi inanikanganya pale ninapojua ya kuwa chama hiki
ndicho chenye hatamu na ndicho chama tawala. Kimekuwa mstari wa mbele katika kujikita uongozini kwa juhudi zote kama vile kusukuma greda kwa kutumia fito.

Lakini kuna chama hiki

Kimekuwa kikishutumiwa sana na chama kileee juu ya kuwa kinataka kuleta uvunjifu wa amani kwa kuwaeleza watanzania waliolala usingizi mkubwa ya kuwa wananyonywa na kupelekwa pabaya. Na kuwa serikali yao haina jipya la kuwaletea kimaendeleo baada ya miaka 50 ya kuwa madarakani, hivyo waamke na kuchagua chama kitakacholeta maendeleo. Mimi nahisi huo ndio ukweli na maana ya upinzani. Kukosoa chama tawala pale kinapokosea.

Sasa huyu ndugu

naye anakuja juu na kumkashifu mpinzani wa serikali. Huyu ndugu anadai tena ati Chama chenye mamlaka ya wananchi kinataka kupinduliwa na chama kingine kwa kuwaamsha waliolala usingizi, ati wakiamka kwa ghafla watakuwa na hasira na mtawala wao kwa kugutuka kuwa walipokuwa wamelala, walikuwa wanapigwa bakora sana kama vile hawana akili nzuri..
Huyu ndugu kaungana na mwingine ambaye ana bendera ya bluu ambayo haipatikani mitandaoni na kumshambulia huyo anayekuja kwa nguvu za uma. Naye anadai mwenye dola anataka kupinduliwa kwa staili ya kuwaamsha watu wajue ya kuwa wanatembea bila nguo barabarani.
Sasa hapo ninachanganyikiwa, kwani sijui chama tawala ni nyundo au ni antenna.
Kama wewe unajua kisayansi, basi nielezee!!
Angalizo: Mimi sio mwanasiasa, ila ni mpenda maendeleo na ukweli


Thursday, March 10, 2011

Umakini wa Watanzania!


Waziri wa nishati na madini, Mhesh Ngeleja, wa tatu kutoka kushoto akisikiliza kwa makini hoja katika mkutano mmojawapo wa kimataifa.

Kulia kwake yupo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mh. Kikwete.

Picha kutoka kwa Mnyonge Mnyongeni....

Thursday, March 3, 2011

Uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa waishtua Rwanda

Rais Sarkozy amefanya uteuzi mpya wa waziri wa mambo ya nje na kumteua Allain Juppe.

Juppe alikuwa na wadhifa huo huo wakati wa mauaji ya kimbari yaliyoikumba Rwanda mwaka 1994 na inasemekana alikuwa anaiunga mkono kwa nguvu serikali iliyokuwa madarakani Rwanda wakati wa mauaji ya watutsi.
Alidumu katika wadhifa huo hadi mwaka 1995.

Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda, Bibi Mushikiwabo, ameonyesha wasiwasi na kutofurahishwa na uteuzi huo ukuzingatia ya kuwa Rwanda na Ufaransa zimefufua mahusiano chini ya miaka 2 iliyopita, baada ya serikali ya Rais Kagame kuisusia Ufaransa kwa kile kilichokuwa kinaelezwa ya kuwa Ufaransa ilihusika moja kwa moja na uchochezi wa mauaji ya Kimbari ya watutsi, na hii ilipelekea Rwanda kubadili hata na lugha rasmi ya matumizi na kujiunga na jumuiya ya madola na kuanza kuzungumza na kufundisha shuleni kiingereza badala ya kifaransa.

Kumekuwa na wasiwasi ya kuwa watu watatoneshwa vidonda vya mauaji ya 1994 kwa uwepo wa waziri huyu kwenye wizara ile ile ambayo iliacha watu takribani milioni moja wakiuwawa kwa visasi.