Wednesday, December 28, 2011

Tatizo la Mafuta Tanzania

Bado ninajiuliza hili tatizo la upatikanaji wa mafuta Tanzania, ni tatizo la kweli au ni janja tu ya wanaojishughulisha na biashara ya mafuta kunufaika zaidi? 
  
Kwa nini matatizo yawe yanatokea katika vipindi ambapo watu ndio wanahitaji mafuta kwa wingi, na kwa nini linakuja pale bei ya EWURA inaposhuka tu. 
 
Bado najiuliza, mbona siku za nyuma tatizo hili lilikuwa halitokei? 
 
Kila la heri katika maandalizi ya mwaka mpya wa 2012!!!!

Friday, December 2, 2011

Waziri Mkuu wa Zimbabwe Tsvangirai Aachana na mke Mpya Baada ya Siku 12 tu

Waziri mkuu wa Zimbabwe, Morgan Tsvangirai, ameachana na mkewe ambaye ni mfanyabiashara tajiri nchini Zimbabwe Bi Lorcadia Karimatsenga Tembo mwenye miaka 39. 
 
Anadai chanzo ni kuingiliwa na vyombo vya usalama na kujaribu kumchafua kisiasa! Pia, anamshuku mkewe kuwa alikuwa anashirikiana na wana usalama ili kupanga njama za kumharibia kisiasa, kwani... at mkewe alikwenda kwa wazazi wake(Mke) bila kumtaarifu Waziri Mkuu (Mume). Hivyo kutokana na hayo, uhusiano wote umevurugika na hauwezi kusuluhishwa tena. 
  
Inadaiwa alikuwa amekwishalipa dola za kimarekani 36,000 na ng'ombe 10 kama mahali, lakini kwa kuvunja ndoa hii imebidi alipe dola 10,000 kama fidia kwani mke wake huyo alikuwa tayari ni mjamzito na alikuwa na watoto mapacha.

Pata habari kwa kimombo kwenye link hii

Thursday, December 1, 2011

Tujiepushe Na Maambukizi ya UKIMWI



Leo ni siku ya UKIMWI Duniani.
Tunakumbushana tu kujiepusha na vitendo au vyanzo vinavyoweza kuendeleza kueneza UKIMWI Duniani. 
  
Take Care for yourself and your loved ones!