Thursday, May 27, 2010

Uchokozi wa Venus Williams


Hivi karibuni Venus Williams alizusha gumzo pale alipoingia kwenye mashindano ya tennis akiwa amevaa bukta inayobana ambayo ina rangi karibu sawa na ngozi yake, kiasi kwamba waliokuwa wanamuangalia katika michapo ya tennis walikuwa wakipata hisia kama vile hajavaa kitu.
Kuna baadhi walilalamika sana!
Kama una macho mazuri kama ya kwangu utaiona bukta vyema, lakini ukiamua kutokuiona, basi utaishiwa na la kusema.

Monday, May 17, 2010

Mumhery: Ninakukubali Sana



Wanablog wanaonivutia kwa kuitangaza Tanzania vyema ni wengi.

Mmoja wa wanaonivutia sana ni Mumhery ambaye yupo pichani hapo juu na ambaye anaishi Japan.

Pamoja na kuwa anajishughulisha kujikimu na maisha, lakini bidhaa zake ambazo ni za ubunifu wa hali ya juu hulitangaza vyema bara la Afrika hususan Tanzania.

Makala zake za biashara na matukio, hazikosi kionjo cha nyumbani, na cha kufurahisha zaidi, huwatumia wajapani wenyewe kwa kudhihirisha ya kuwa mavazi hayo yanawapendeza pia.

Natoa changamoto kwa watanzania wengine kumuunga mkono Mumhery kwa juhudi za kukuza uchumi wetu, wa nchi na kuitangaza Tanzania.

Mumhery hongera sana!

Monday, May 10, 2010

Hongera Chelsea


Nawapa pongezi wapenzi wote wa Chelsea kwa kuweza kutwaa ubingwa kwa kubahatisha!!!

Msinishambulie kwa hilo.

Mabao 8 - 0 ni mengi lakini mkicheza na timu yenye wachezaji pungufu... mlikuwa na haki ya kuwabamiza.
Man. united kazeni buti tena, msimu ujao una kazi kweli kweli.

Gunners... msimu wenu kuvunja watu miguu sasa.. ha ha haaaa

Tuesday, May 4, 2010

With a Light Touch

A thief-catching-machine was invented in Japan and tested in various parts of the world.
The results were very interesting!

In USA, it caught 30 thieves in 30 minutes;
In UK, it caught 20 thieves in 35 minutes;
In Kenya, it caught 30,000 thieves in 20 minutes and;
In Nigeria, the machine itself was stolen in just 5 minutes!!!