Thursday, November 11, 2010

Uchaguzi wa Spika Tanzania... Ni Ujanja tu au?....

Inaelekea kuwa vurugu, mipasuko na vidonda vya uchaguzi bado havijapona!!

Suala la msukumo wa kumpata spika wa Bunge la Tanzania unaingia sura mpya mara baada ya CCM kuwachagua wanawake tu kushindanishwa,

Binafsi, nalipongeza suala hili, kwani inaonekana kama vile inajali wanawake, lakini unaweza kukuta ukweli ni kuwa wameona hao mafahali waliokuwa wanatonyana kwenye vyombo vya habari hawawezi kukaa zizi moja iwapo mmoja watampa nafasi ya kukaa juu ya mwingione, ndio maana wakateua wananwake tu! Kama misingi ilikuwa ni ya mtazamo huu, basi bado CCM hawakuwa na mpango wa kuteua wanawake, isipokuwa kuwageuza jamvi la kuficha uovu wao kwa kuwaendesha kwa remote :-(

Kuna wengine waliopendekezwa tulishawasahau kwenye nyanja za siasa... lakini mara wameibuka katika kugombea uspika....sasa hapo kweli sio kwamba wamepanga kwa makusudi mtu fulani kwa matakwa yao?