Thursday, January 21, 2010

Mteleza Theluji Amwaga Radhi Nje Nje


Dada mteleza kwenye theluji wa Uingereza, Gillian Cooke, amepata kisago pale alipokuwa anajiandaa kuchupa katika mashindano ya kuteleza kwenye theluji mara baada ya nguo yake aliyovaa kufumuka kwa nyuma na kumwaga wazi wazi makalio na G-string yake nyeusi.
Bahati mbaya au nzuri hakugundua hii kasoro mpaka alipokuwa amemaliza mtelezo wake ndio kwa tahayari akagundua usumbufu huo ambao ulinaswa live na kamera za waandishi wa habari.
Hili ni fundisho kwetu tupendao kuvaa skin tight, tena za mtumba. Kuna siku zitakuaibisha

Tuesday, January 19, 2010

Haiti Aid Overwhelm the Actual Supply


Haiti imekumbwa na tatizo kubwa la tetemeko la ardhi.

Wakati naangalia TV nimepata na sikitiko kubwa kuona watu wakifa ndani ya majengo walipokwama kwa sababu tu ya vifaa duni kuwaokoa.

Pia misaada mingi imekuja lakini imeshindwa kuwafikia walengwa kwa sababu ya ubove wa miundo mbinu iliyofuatia haribiko la tetemeko.

Tatizo jingine jipya ni kuwa hakuna anayesimamia ugawaji wa misaada, kila mtu anajifanya yeye ndio kinara. Wakati USA imehodhi uwanja wa ndege na hivyo kufanya ndege za misaada kutoka sehemu nyingine kushindwa kutua, Umoja wa mataifa umekuwa unajifanya ndio unasimamia ugawaji wa chakula huku ukiwa hauna jitihada zinazo onekana kwa kugawa chakula.

Naye Rais wa Haiti anadai yeye ndio kiongozi wa shughuli zote, wakati hana meno hata ya kuamua nii kiende wapi na nini cha kufanya.

Mashirika mengine yanafanya kazi kiaina bila kuwa na mipangilio ya pamoja, lakini yanashukuru kuwa hakuna masuala ya kisiasa katika kutoa misaada wakijaribu kulinganisha na sehemu kama Darfur - Sudan na kule Myanmar walipojaribu kwenda wakati wa majanga.

Wanaoumia zaidi ni wananchi wa kwaida, inasikitisha sana kwa kweli

Soma hapa kwa maelezo

Tuesday, January 12, 2010

Admirable Michelle Obama

I always admires Lady Michelle Obama..

Huyu mama alistahili kuwa mwanamitindo, maana anajua kuchagua nguo za kuvaa, na sijui kama huwa anarudia nguo.

Ninatamani siku moja ningepata fursa ya kutembelea ward-robe yake nikajionee mitindo mbalimbali ya nguo zake.

Wednesday, January 6, 2010

Uchumiiiiiiii


Ugonjwa mwingine kuna wakati unaweza kuwa kivutio au kuleta visa na mikasa
Hapo sijui kama mtoto anahitaji kufungwa na mbeleko!!

Tuesday, January 5, 2010

Vazi rasmi la Kidini


Mtoto mdogo akiwa katika kundi la wanawake wa kiislamu.
Sijui kwa nini yeye naye hakuvishwa nguo za namna ile.. kama ya watu wazima

Friday, January 1, 2010

Heri ya mwaka mpya wa 2010

Nawatakia heri ya mwaka mpya 2010 kwa watu wote haswa wapenzi wa blogu.

Nipo kijijini napumzika, mtandao ni kazi kweli kuupata.

Ngoja tukusanye nguvu turudi tena kwenye ulingo.