Thursday, April 21, 2011

Salamu za Juma Kuu na Pasaka

Wakati tunaendelea kuingojea sikuu ya Paska, tunapaswa kuwa wema kwa matendo na kukumbuka mateso ya yule watu wengi wanaomwaminiya ya kuwa alikubali kuteswa kwa ajili ya kiumbe binadamu. 
  
Wakati tunapotafakari picha hii na maajabu yake, basi tujiandae vyema kuupokea ufufko wake kwa matendo mema. 
 
Nawatakia kila la heri katika Ijumaa kuu, paska na jumatatu ya paska. 
  
Mbarikiwe sana

Friday, April 15, 2011

Maana ya Kujivua Gamba ni Nini?

Bado sijaelewa Dhana ya kujivua gamba.

Natazama... kama vile kupaka rangi nyumba bila kubadili chochote ndani, au kama vile nyoka anavyojivua gamba lake na kuondoka akiwa na kila kitu chake ikiwa ni pamoja na sumu, tabia, ukubwa, viungo na uwezo wake wa kizazi bila kubadili hata na jinsia.

Sasa wenzetu wamejivua gamba kivipi?

Mh! Nawatakia kila la heri na mafanikio, yote iwe kwa mema ya Tanzania na watu wake!