Monday, June 28, 2010

Likizo na Kombe la Dunia

Jamani hili kombe la dunia naona ni balaa tupu!

Hakuna kinachofanyika, watu kukaa na kukodolea macho runinga na kupiga mayoweeeee.

Mimi nina mapenzi na michezo, lakini michezo hainuchukulii muda wangu wote. Ninasikitika kuona tumeahirisha mitihani ya majaribio eti kwa sababu watu hawataki kukosa kuona kombe la dunia. Hivyo hawawezi kusoma kujiandaa na test!!

Penye wengi, hapakosi neno, na pia wengi wape. Tumepata likizo bila kutarajia....

Tunatumaini kurudia kama kawaida katikati ya mwezi wa julai.

Nawatakia wapenzi wa mpira kipindi chema, kwani sina zaidi la kusema.

Ghana hoyeeee!!!!!

Thursday, June 24, 2010

Williams: Perfect sisters

Happy sisters

Lovely sisters

Champions sisters

Energetic sisters

They love tennis

Wednesday, June 2, 2010

Watanzania Tumerogwa???

Nina maswali mengi sana ninajiuliza kwa nchi yetu ya Tanzania....
Yanakuja haswa pale uchaguzi wa Rais na wabunge unapokaribia.


Kuna kuwa na visa vingi vya watu kushikana uchawi, mara huyu kamroga huyu.
Watu wanapotangaza azma ya kugombea mathalani ubunge, utashangaa aliye na jimbo anaanza kugaagaa na vyombo vya habari, mara apeleke vitisho na kumtaka yule anayetaka kugombea ati ajitoe, au asichukue form ya uchaguzi

Kana kwamba hiyo haitoshi, utaskia vifo vya ajabu na watu wakishikana uchawi.
Lakini si uongo, nasikia wakati huu waganga wa jadi wana soko zuri sana, na ndio wakati wao wa kivuno toka kwa politicians wajinga.
Naogopa kutamka jina la wananchi ambao huwapa wanasiasa wajinga kura, labda wewe msomaji unaweza kuwa na jina zuri.
Jana nilimsikia Pinda akisema hivi watanzania tumerogwa????? Kwa sababu fursa zote tunazo za kujiendeleza, mali ghafi, madini, mito, maziwa, vivutio, amani, viongozi safi na wazuri ( cha ajabu huwa hawachaguliwi hao) nk
Lakini hatuna hata chembe ya maendeleo, nami naongezea, hao hao mafisadi na wezi ndio tunawapa kura ati, na wala hata hatuchoki.
Hivi ni kweli tumerogwa???
Kwa nini tuna amini bila ushirikina basi hatuwezi kushinda uchaguzi?
Mimi kwa kweli sijarogwa, wale wajinga ambao huuza kura zao kwa pilau tu ndio waliorogwa.
Nimetema mate pwaaaa!