Wednesday, December 16, 2009

Monday, December 14, 2009

Michezo mingine Kwa Akina Dada!!


Mimi ni mpenzi sana wa chokleti, nikiiona mate hujaa mdomoni.

Lakini nilipoona haya mashindano ya kupigana mieleka huku mwili mzima ukiwa umepakawa chokleti, ....... nilisikia kama vile kutema.
Mavazi wanayovaa pia... ambayo ndio kama ndoano ya kumwangusha mtu, nisikilizie ikivutwa watu wanavyoachwa @*%?


Hawa ni akina dada huko Belarus wakiwa katika mieleka hiyo ya ukichaa, ati na watazamaji wapo kushuhudia, na tena sijui wanalipia!!

Picha kwa hisani ya travelNews

Wednesday, December 9, 2009

Viongozi wa Tanzania na Uhuru wa wa-Tanganyika

Mimi huwa sipendi kabisa kuzungumzia mambo ya politiki, lakini kwa sababu Tanzania inasheherekea miaka 48 ya uhuru wake...

Watanzania wengi wamekuwa na mtazamo tofauti na viongozi wao. Mfano mzuri ni kamahuyo ng'ombe dume au bull, ambaye anafananishwa na kiongozi mbele ya watu, ya kuwa yeye anataka kuwajeruhi wananchi wanomtunza kwa kumwekea kibanda asishambuliwe na simba usiku, na wakati huo huo huyo bull yeye anawaona wananchi kama kikaragosi, na kuwakimbiza kila anapowaona na kuwajeruhi, bila kufikiria ya kuwa ni hao hao watu ndio wanaomlinda kwa kumpa lishe,makazi na matibabu.

Fikiria hilo li-bull likikuumiza, linajali? au litatafuta mwingine wa kujeruhi. Ndio raslimali zetu zinavyo jeruhiwa

Ni wazo tu la siku ya uhuru.

Sunday, December 6, 2009

Vazi la skeleton



Mambo ya ubunifu wa mavazi mh! Sijui designers wamekosa cha kubuni!!

Hapa ni maonyesho ya mavazi ya ki-aina, nguo hii imetengeenezwa na kunakshiwa kwa picha ya mifupa (skeleton). Sifahamu mtu ataivalia wapi nguo kama hii

Kazi ipo

Thursday, December 3, 2009

Tiger Wood - Mzinzi?



Inasemekana Tiger Wood alipopata ajali ya gari hivi karibuni, alikuwa ameyoka kupata kipigo kutoka kwa mkewe.
Sababu ni kuwa amekuwa na uhusiano wa kimapenzi nje ya ndoa yake.
Mkewe, Elin Nordegren ambaye ana miaka 29 sasa (tunashea birth day) na mwenye watoto wawili, zamani alikuwa mtu wa mitindo na urembo huko kwao Sweden, inasemekana alikasirishwa sana na kitendo hicho.



Elin, Enzi hizo za u-model




Wood ambaye ni mkimya sana, inasemekana hajaweka wazi habari hii, ingawa kuna fununu kuwa ni kweli kwa namna fulani alikiuka kiapo!
Kwa ajali hiyo Tiger amesababisha hasara ya dola 3,500 kwenye gari na mti alio-ugonga!!

Haya ndio matatizo ya kuwa mtu maarufu, watu wanakufuata kama inzi ....

Tuesday, December 1, 2009

Sexy designs!



Halafu mtu unasingizia ati umevaa sketi!!!
He eh he heeee



Hivi nikijaribu nguo kama hizi itakuwaje, figure yangu, mhhh sijui

Friday, November 27, 2009

Michoro inavyoremba Uso na Mwili



Ahaaaa



Sio lazima kutumia gharama kubwa kuupamba uso na kuwakaribisha vibaka kukupora.

Very simple, hata kwa watoto wanapendeza, jaribu kufanya hivi siku ya sherehe ya mwanao ya kuzaliwa, utamwona jinsi atakavyo furahia, he he heee

Thursday, November 26, 2009

Hmm!! Men designs!



I was attracted by these men's fashion which I came accross this website



Ni za ajabu , lakini nafikiri watu wakizijaribu kwenye award fulani wanaweza kuwa gumzo la siku



Designer ni John Galliano, kwa wale mnaomfahamu.

Wednesday, November 25, 2009

Rihana: Kipindi cha mpito



Rihana kama unavyomuona hapo juu, yupo katika kipindi kigumu, labda pia cha furaha kwa kuachana na rafiki yake katili kama wanavyomuita wengine Chris Brown.

Anajiandaa kuporomosha vitu vipya, ingawa amechelewa kidogo kuvitoa kama ilivyotarajiwa.

Mtakumbuka Chris alishitakiwa baada ya kumjeruhi vibaya Rihana katika mzozo, na watu walimshauri Rihana kuachana naye.

Monday, November 23, 2009

Tuwajibike jamani


Wikend imekwisha! Burudani imetosha, na umeliwazika vya kutosha.
Ni wakati wa kujenga nchi yako.
Jumatatu njema

Sunday, November 22, 2009

Vimini: Vinavutia au humpendezesha mdada!!


Kuna dhana moja ambayo watu wengi wanadau mwanamke kuvaa nguo/sketi fupi huwa anapendeza, na hasa anapokuwa ana umbo pana.
Swali ninalojiuliza, ni kweli huwa anapendeza au anakuwa kivutio kwenye macho ya wanaume?
Wazungu wengi huwa si wenye maumbile yenye hips pana, pale wanapovaa nguo fupiama dada hapo juu niliyebahatika kukutana naye huwa hawawapagaishi wanaume.
Jaribu kufikiria mdada mbantu hapo chini akivaa kimini kama hiki atapendeza au kuvutia?
Kazi kwako

Friday, November 20, 2009

Hips, Hips na mahips

Unene umekuwa unahusishwa na magonjwa ya moyo, lakini wataalamu wanasema si kila unene unaweza kuleta magonjwa hayo. Unene wa hips na matako pekee hauna madhara na wala hakuna haja ya kumsumbua mtu na kumwambia apunguze mlo. Pia inasemekana mapaja kuwa mapana ni njia kinga ya magonjwa hayo ya moyo.
Ila unene wa tumbo yaani kitambi ndio mbaya.

Inasemekana wanawake wenye hips pana pamoja na kwamba wana usalama kwa magonjwa ya moyo, lakini waume zao wapo katika hatari ya kupata magonjwa ya moyo, kwa sababu ya wasiwasi, hasa wake zao wanapolazimika kwenda kwenye semina au warsha na kulazimika kukaa huko kwa zaidi ya siku 2, huku nyuma wanaume viroho huwadunda sana na kusababisha matatizo ya moyo.

Sijui wewe unasemaje!?

Picha: Imebanduliwa kutoka kwa Masangu

Thursday, November 19, 2009

Nashukuru kuingia humu

Nafahamu mwanzo ni mgumu, lakini najua wadau mtaniunga mkono na kunisapoti ili niwe kama nyinyi.

Nitatembelea blogu zenu kujifunza mengi kutoka kwenu, naomba msinichoke.
Pia nawakaribisha sana, msiudhike na vituko hapa kwenye blogu, kila kitu ni kuelimishana, kinachoudhi, ni funzo kwa watu kwamba tusifanye hayo mambo.