Tuesday, January 25, 2011

CCM si Shwari Hata Chembe?


Kuna fununu kuwa hali ya kifedha ndani ya chama cha mapinduzi aka CCM iko tete hasa baada ya kukumbwa na rungu la kupoteza nafasi nyingi za ubunge, na hivyo kupungua kwa kiasi kikubwa cha ruzuku ya kila mwezi.
Pia inasemekana inasakamwa na madeni katika uchaguzi uliopita na kufanya viongozi waanze kuhaha kuokoa jahazi. Inasemekana shinikizo la kujilipa kupitia Dowans ndio nia hasa ya kupata pesa kwa ajili ya kuendesha shughuli za chama, kulipa madeni na pia kukatia rufaa baadhi ya matokeo ya uchaguzi uliopita katika sehemu ambapo CCM iliangukia pua!
Pia inaaminika ya kuwa wabunge wengi wa CCM wakati wa uchaguzi walijigharimia wenyewe kwa ahadi kuwa watarejeshewa baada ya uchaguzi, kwani ruzuku za majimboni, zilielekezwa kwenye nguvu ya kugombea urais!! Lakini kutokana na kuanguka kusikotegemewa kwa CCM, hali imekuwa ni mbaya.
Pia kuna mnong'ono kuwa kuna baadhi ya makatibu na wenyeviti wa kata, na hata wilaya, malipo yameanza kuwa magumu, na kuna watu wanasingiziwa kukihujumu chama wakati wa uchaguzi ili wapate kisingizio cha kuwacheleweshea mishahara yao au hata kuwarusha!
Inasemekeana kuna wimbi la mgogoro litafumuka ndani ya kijani/njano hivi karibuni iwapo hali hii tete itaendelea, ndio maana wanahaha kulipa haraka Dowans.
Haya ni maono tu, usiulize ushahidi!!
Picha ya bendera mbinuko kutoka kwa Matukio Daima

Thursday, January 20, 2011

Jamani, Nipo

Wapendwa wangu!!!

Mwaka huu, sijui kwa sababu ulianza na 1.1.11 nami ilikuwa siku yangu ya kuzaliwa, basi sijui nilichanganyikiwa!!!

Magimbi na matembele naona yalikuwa yamenilevya, hata hivyo yote ni heri, mimi ni mzima na buheri wa afya.

Nina matumaini nanyi pia mu wazima kabisa.
Nawashukuru kwa uvumilivu wenu, na cha muhimu kupita mara kwa mara kusalimia nyumba iliyokuwa haina mwenyewe.

Mungu awabariki sana!!
Tupo pamoja