Monday, July 16, 2012

Kero Mitaani


Iwapo wewe utaona kuwa na ng'ombe wamejaa barabarani na kukuzuia kupita ukiwa maeneo ya vijijini, basi wenzetu mabata ni kero mijini.

Nawatakia siku njema!

Monday, May 14, 2012

Tuesday, April 24, 2012

Hello Bloggers!

Wapendwa hamjambo!!
Kimya kikuu kina mshindo jamani.
Ninatarajia kuanza kujikongoja na mambo ya blogging.
Mitihani na masomo kwa ujumla yalikuwa yamenibana sana tena sana.

Tupo sote

Tuesday, February 14, 2012

Monday, February 13, 2012

CHADEMA Chaanza kupata "Umaarufu" Zanzibar

Matokeo ya uchaguzi mdono wa jimbo la Uzini, Zanzibar yameanza kutoa picha tofauti za kisiasa visiwani Zanzibar, mara baada ya mgombea wa CCM kuibuka kidedea kwa kuzoa zaidi ya asilimia 90 ya kura zote zilizopigwa. 
  
Kulikuwa kunatarajiwa kuwa na mchuano mkali kati ya CCM na CUF, lakini imekuwa kinyume kwani ushindi wa CCM kupitia kwa mgombea wake Mohamed Raza ambao ulikuwa ni wa mteremko, alifuatiwa na Ally Mbarouk Mshimba wa CHADEMA na mgombea wa CUF kushika nafasi ya tatu. 
  
Sina hakika nini kinachoendelea huko Zanzibar, lakini kwa matokeo hayo, yanaashiria kuwa CHADEMA huenda kikawa chama kitakachokuwa kinaongoza kwa upinzani huko Zanzibar. 
  
Kwa upande wa Bara, nina wasiwasi kama CUF itaendelea kuwa na wafuasi wengi, kwani hata leo kuna wanachama zaidi ya 1,000 wamerejesha kadi zao za CUF kwa kutoridhishwa na mwenendo wa chama chao. 
  
Wakati ni ukuta, nafikia tamati kwa leo! 

Tuesday, February 7, 2012

Bunge Letu Linavyoonekana kwa Sasa

Mhesh. Anna Kilango Malecela akifuatilia kwa makini mjadala ndani ya bunge hivi karibuni. 
  
Inaonekana wabunge wamesusia posho mpya!

Wednesday, January 25, 2012

Mgogoro wa Wizara ya Afya na Madaktari!!!

Tanzania yetu ni nzuri sana. 
 
Viongozi wanajiamulia wanavyotaka wakitegemea walio chini yao kukaa kimya kama vile hawaoni wala hawasikii. 
Mtu akikunyima haki yako anataka ufunge domo lako. ati uking'aka kidogo, basi anatishia kukuumiza au kukutimulia mbali kama vile vumbi, na wala asitake kujua utaangukia wapi na nani utaenda kumchafua kwa kumuangukia, kwani umetimuliwa mahali na kufikishwa pengine pasipo matarajio yako. 
 
Huko unakotua, ukimuangukia mtu, anakukung'uta huku akitukana kama vile wewe ulipenda, au alifanya makusudi kuanguka mahali ulipoangukia. 
 
Ikiwa umeona umeumizwa kwa adhabu uliyopewa, ambayo hukustahili kuipata, bali yule aliyekupa adhabu hiyo ndio alitakaiwa kulaumiwa, basi yeye ndio anakuwa wa kwanza kwenda kulalama kwenye vyombo vinavyopaaza sauti ya kuwa anakushangaa kwa nini unapiga kelele wakati yeye hata hajakugusa!! Kama vile anawaowaambia ni majinga tu na ambayo hayaoni kitu!!. 
  
Vurugu hizo sasa zinakuwa za mafahari wawili, wao hawaumii kama vile nyasi zisizo na hatia, tena ambazo hupendwa sana na mafahari hao ili waweze kuishi, basi ndio wanazichakaza kwa mvutano wao, huku fahari mkubwa ambaye ndio mchokozi, akitaka kuonekana ndio mwema na anayejali uwepo wa nyasi wanazozikanyaga!!! 
  
Huku huyo fahari mkubwa akijua ya kuwa hata wakizichakaza hizo nyasi, yeye nyasi zake zipo ughaibuni, tena zinarutubishwa zaidi zikimsubiri yeye, na yule fahari mdogo hana zaidi ya kukubali kukanyagwa mabegani mwake, ili fahari mkubwa apande na kuingia kwenye pipa ili akale nyasi nzuri akimuacha fahari mdogo akilamba zilezile nyasi walizozikanyaga...... 
  
Ama kweli... huu mgogoro wa madaktari na wizara yao ukome. Wanaoumia ni wagonjwa!!!