Wednesday, December 1, 2010

Upinzani Tanzania Maana Yake ni Vita vya wenyewe kwa wenyewe

Upinzani Tanzania, unaelekea kupoteza uelekeo kwa sasa.

Ule msingi wa upinzani kufanya juhudi ya kuiangalia na kuikosoa serikali (watch dog) sasa ujaelekea kupata doa.

CHADEMA ambacho ni chama kilichokuwa kinatarajiwa na wengi kuonyesha cheche za moto, badala ya kujipanga kutetea maslahi ya nchi, kimeanza kugeuka na kuanza kuwashiana moto ati kwa nini watu hawakwenda bungeni na kudai ni watoro, kwa hiyo wajieleze kimaandishi.

Mimi naona ni ubabe usio na maana sana, nafikiri ulikuwa ni wakati wa CHADEMA kushikamana na kupanga mikakati ya kuleta maendeleo kuliko kuanza kunyoosheana vidole.

Hii inatupa picha mbaya kama kitaingia madarakani, kwani kinaelekea kuwa chama cha migogoro na vurugu.

Kina wajibu wa kutulizana kuliko kuleta mkanganyiko na mwishowe kuporiomoka kama NCCR mageuzi ilivyoporomoka wakati uleee wa Mrema vs Marando.

Jameni, mtusaidie nyieeee

No comments: