Monday, June 28, 2010

Likizo na Kombe la Dunia

Jamani hili kombe la dunia naona ni balaa tupu!

Hakuna kinachofanyika, watu kukaa na kukodolea macho runinga na kupiga mayoweeeee.

Mimi nina mapenzi na michezo, lakini michezo hainuchukulii muda wangu wote. Ninasikitika kuona tumeahirisha mitihani ya majaribio eti kwa sababu watu hawataki kukosa kuona kombe la dunia. Hivyo hawawezi kusoma kujiandaa na test!!

Penye wengi, hapakosi neno, na pia wengi wape. Tumepata likizo bila kutarajia....

Tunatumaini kurudia kama kawaida katikati ya mwezi wa julai.

Nawatakia wapenzi wa mpira kipindi chema, kwani sina zaidi la kusema.

Ghana hoyeeee!!!!!

No comments: