Kwa nyie mnaosikiliza kampeni za uchaguzi....
Hivi mmekwisha tafakari wenzetu wanayoahidi?
Kila mtu anaimba wimbo wake, sina hakika kama kila mtu atatimiza hayo kwenye miaka mitano anayo omba tumpe kura zetu ati atuwakilishe.
Mimi nitajenga uwanja wa ndege wa kimataifa katika kila wilaya!!!!
Mimi nitatoa elimu ya bure tangu mtoto akiwa tumboni kwa mama yake mpaka atakapo ng'oka jino la mwisho la uzeeni!!!
Mimi nitajenga meli mpya kila mto hapa Bongo, ili watu wasiliwe na mamba tena!!!!
Mimi nitahakikisha kwa muda wa wiki 2 tu, jimbo langu lote litakuwa na maji ya uhakika kwa mwaka mzima na barabara zinazopitika kila siku. (Hapo nina maana ya waenda kwa miguu, na maji ya uhakika mvua zitakapokuwa zinanyesha)
Mimi nitatoa ajira kwa watu wote, ukipata ujauzito, njoo umwandikishie mtoto wako kazi kabisa, ili akizaliwa anaanza ajira rasmi moja kwa moja...
Mimi nitatokomeza ufisadi na kilimo cha bangi kila mahali hata ikulu kama inalimwa huko!!!!!
Huo ndio mwelekeo wa kampeni, kama unatafakari, utang'amua yote, kwa jinsi ambavyo umeona mifano yangu, basi jua mwananchi wa kawaida ndio anaelezwa ahadi za namna hii.
Monday, September 27, 2010
Monday, September 20, 2010
Wednesday, September 15, 2010
Uchaguzi Tanzania:Maswali maswaliii
Kwa haraka haraka
Nimekuwa nikfuatilia kampeni za siasa, kwani sitaki kufanya makosa wakati utakapowadia wa kumchagua kiongozi wangu wa baadaye, ukizingatia ya kuwa hii itakuwa ni mara yangu ya kwanza kushiriki katika zoezi zima la kupiga kura za kuchagua viongozi wa nci yetu,
Nimekuwa nikisikiliza kwa makini sera za wagombea mbalimbali na kuzipima kama zina ukweli, ushawishi, na pia kuangalia kama kweli zinatekelezeka au ni changa la macho.
Nahisi naanza kukata tamaa, kwani wanasiasa au wagombea nafasi za kisiasa badala ya kuhubiri sera za vyama vyao, wamekuwa mstari wa mbele kusikiliza mwenzie alisema nini, na wao kusema ya kwao kutokana na wengine walichosema hapo awali, na mwisho hakuna kampeni tena bali ni kupeana vidonge na kujibu mapigo!!!!!
Sie tunaotaka kupima sera tumejikuta tukipima nani ni bingwa wa kujibu mashambulizi, na mara ,,, hatimaye zoezi la kupiga kura litafika.. sasa hapo tutampigia kura nani?, nahisi hatutakuwa tumempata kiongozi atakayekidhi tulichotaka kusikia kabla ya kuamua.
Mpaka sasa mimi naona wengi ni wahuni na matapeli tu. Wanabembeleza wachaguliwe kwa matakwa yao binafsi. Na kwa maono yangu, naona vyama vimeelekeza nguvu na pesa nyingi kwa wagombea urais, kwani kutumia helikopta nyingi na magari utitiri kwa mgombea mmoja, wakati wagombea ubunge na udiwani wakiswaga lami ni kuonyesha ishara ya uchoyo na unafiki tu
HATUDANGANYIKIIIIIII
Nimekuwa nikfuatilia kampeni za siasa, kwani sitaki kufanya makosa wakati utakapowadia wa kumchagua kiongozi wangu wa baadaye, ukizingatia ya kuwa hii itakuwa ni mara yangu ya kwanza kushiriki katika zoezi zima la kupiga kura za kuchagua viongozi wa nci yetu,
Nimekuwa nikisikiliza kwa makini sera za wagombea mbalimbali na kuzipima kama zina ukweli, ushawishi, na pia kuangalia kama kweli zinatekelezeka au ni changa la macho.
Nahisi naanza kukata tamaa, kwani wanasiasa au wagombea nafasi za kisiasa badala ya kuhubiri sera za vyama vyao, wamekuwa mstari wa mbele kusikiliza mwenzie alisema nini, na wao kusema ya kwao kutokana na wengine walichosema hapo awali, na mwisho hakuna kampeni tena bali ni kupeana vidonge na kujibu mapigo!!!!!
Sie tunaotaka kupima sera tumejikuta tukipima nani ni bingwa wa kujibu mashambulizi, na mara ,,, hatimaye zoezi la kupiga kura litafika.. sasa hapo tutampigia kura nani?, nahisi hatutakuwa tumempata kiongozi atakayekidhi tulichotaka kusikia kabla ya kuamua.
Mpaka sasa mimi naona wengi ni wahuni na matapeli tu. Wanabembeleza wachaguliwe kwa matakwa yao binafsi. Na kwa maono yangu, naona vyama vimeelekeza nguvu na pesa nyingi kwa wagombea urais, kwani kutumia helikopta nyingi na magari utitiri kwa mgombea mmoja, wakati wagombea ubunge na udiwani wakiswaga lami ni kuonyesha ishara ya uchoyo na unafiki tu
HATUDANGANYIKIIIIIII
Thursday, September 9, 2010
Friday, September 3, 2010
Have a Blessed Weekend
Subscribe to:
Posts (Atom)