Monday, January 2, 2012

Wayne Rooney Alimwa Faini ya Mshahara wake wa Wiki Nzima na Klabu Yake


Siri ya mafanikio katika jambo lolote, ni kuwa makini na nidhamu kwa kile unachokifanya.
Mafanikio katika kazi na michezo yote yanahitaji adabu kubwa kwa kufuatilia taratibu zilizopo, na katuika michezo ni kufuata maelekezo ya kocha. 
Kinyume cha hapo, kinaweza kukugharimu kitaaluma na kimaendeleo. 
 
Ndio maana Mkufunzi mkuu na meneja wa Manchester United Mhesh Alex Ferguson hakusita kuwachukulia hatua kali wachezaji wake watatu ambao ni Wayne Rooney, Darron Gibson na Jonny Evans ambao walitoka pamoja usiku kwenda kwenye klabu kula wakiambatana na mke wa Rooney kwenye siku ya kufungua zawadi (Boxing day) 
 
Adhabu hii ilikuja baada ya kuonekana ya kuwa wachezaji hawa hawakufanya vizuri katika mazoezi ya timu siku iliyofuata na hivyo meneja wao Ferguson kuudhika, na hivyo kutoa adhabu ya kukatwa mshahara wao wa wiki nzima (Wayne Rooney anapokea pauni za Kiingereza 250,000 kwa wiki, yaani zaidi ya TZS 600M), na pia kuondolewa kwenye kikosi kilichopambana na timu ya Blackburn, japo Man-U ilipata kichapo kutoka kwa timu iliyokuwa inashikilia mkia ya Blackburn. 
  
Hakukuwa na taarifa ya kuonyesha ya kuwa walikunywa pombe kupita kiasi wala kufanya tukio lolote la kutia fedheha, lakini adhabu ilikuja kama wembe mkali.
 
Mimi si mfuatiliaji sana wa mpira japo huwa napenda kuungalia, lakini msimamo mkali na adhabu ya kukata kipato cha mchezaji kwa asilimia 25 mara moja kwa kosa moja, inaonyesha jinsi gani watu wapo makini sana katika kuangalia na kulinda mafanikio ya kazi zao. 
  
Je, na sisi tupo tayari kuwa makini sana na kazi zetu? 
Nafikiri siri ya mafanikio ni kuwa makini katika kila tunalolitenda. 
 
Nawatakia juma jema lenye mafanikio 
  
Habari hii ipo BBC

3 comments:

Faith S Hilary said...

Huo mshahara wake wa wiki wala haumpi tabu maana kwake kama hela ya big G tu...

Anonymous said...

Wakati wengine hata kwa miaka kumi hicho kipato hakyanani hatukipati.
Binadamu wote ni sawa na ........ ni moja ha ha haaa

chib said...

Dah!