Tuesday, July 20, 2010

Siasa: Ni upupu wa Kujipakaa au?

Kampeni za uchaguzi karibu zinaanza...

Mie nauita ni mchezo mchafu, kwani utakuta watu wametulia na ni marafiki na kucheka cheka kila mara.

Ukikaribia uchaguzi watu wana anza kununiana na kuitana majina ya ajabu, sijui mavuvuzela, mara watu wanapandikiziana bangi ili mwenzao akamatwe wapete wao tu kwenye uchaguzi.

Wengine sijui wanaenda Bwagamoyo na kuku wa kijani, mara kuku wa samawati... yooote ya nini hiyo.

Mwisho wakati wa kampeni, ni kupakana matope, kutukanana nk nk, yaani utafikiri ni vichaa fulani hivi.

Kwa nini nisiite ni mchezo mchafu...

Tuesday, July 6, 2010