Monday, August 2, 2010

Kura Za Maoni CCM: Vurugu Tupu

Jamani hizi kura za maoni za CCM mbona zimejaa rafu sana...

Kweli chama hiki ni safi au kimejaa uchafu, yaani madai ya hongo, vurugu, na kila aina ya mambo yasiyo kimaadili katika kuomba ridhaa ya kuwakilisha chama ili kupata viongozi yanasikika.

Cha ajabu na watuhumiwa wa ufisadi, kuna wanaojizolea kura nyingi tu. Tutafika kweli?!!!

Nini mwelekeo wa siasa zetu.


Mimi naogopa kabisa. Itabidi niitumie kura yangu vizuri kumchagua kiongozi wa kweli. Wananchi tusiangushane